Thursday 20 September 2012

WAISLAMU KUKUSANYIKA JANGWANI KUPINGA FILAMU YA INNOCENCE OF MUSLIM

Amiri wa Shura ya maimamu Tanzania, Shekh Mussa Kundecha (kulia) akiwa masheikh wa Taasisi ya Umoja wa Wanazuoni wa Kiisilam  wakati wa kutangaza hatua ambazo waislamu watazichukua ili kupinga  Filamu iliyotengenezwa nchini Marekani ya kumkashifu Mtume Mohamad (SAW).Alitangaza
Msimamo uliotangazwa na waislamu hao katika mkutano huo  ni wakufanyika mkutano mkubwa  kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam ambapo waisilamu wote watakusanyika hapo kulaani Filamu hiyo.

Hawa ni waislamu waliohudhuria mkutano huo kwenye msikiti wa Kichangani jijini Dar es Salaam wakati wa Sala ya Ala -asiri leo, wakifuatilia kwa makini matamko na mawaidha ya masheikh mbalimbali

No comments: