Thursday 13 September 2012

KIONGOZI WA FREEMASON KUMWAGIKA LEO CLOUDS TV

Anndy Chande; Gerald Hando aliyeshika kikombe cha chai (kikombe mkononi)
Kinara wa kundi la Freemasons katika eneo la Afrika Mashariki, Jayantilal Keshavji Chande maarufu kama Sir Andy Chande, leo  kuanzia saa 3:00 usiku ataanika mambo mengi kuhusiana na undani wa kundi hilo wakati atakapozungumza na mtangazaji Gerrard Hando wa kituo cha televisheni cha Clouds "The Peoples Station".

Akizungumza kupitia kipindi cha Power Breakfast cha redio ya Clouds FM leo asubuhi, mtangazaji Hando ambaye ndiye aliyefanya mahojiano na Sir Chande, amesema kuwa mambo mengi kuhusu undani wa Freemasons na namna wanavyofanya kazi zao, yameelezewa kwa kina na kigogo huyo wa zamani wa kundi hilo duniani.

Amesema kuwa mahojiano hayo yatarushwa kuanzia leo kupitia kipindi chao kipya kiitwacho "The Interview', ambacho kitarushwa kuanzia leo usiku.

Namna ya kujiunga na Freemasons na mahala liliko hekalu la kundi hilo jijini Dar es Salaam ni miongoni mwa mambo yanayotarajiwa kuzungumziwa na Sir Chande.

Kigogo huyo wa Freemasons amekuwa karibu sana na viongozi wa juu serikalini, wakiwamo marais wastaafu wote wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin William Mkapa na sasa, Rais Jakaya Kikwete.


No comments: