Thursday 20 September 2012

DO YOU KNOW THIS?


A MAN PANNISH HIS WIFE


SIJAUZA ENEO LA KIGAMBONI; JAKAYA KIKWETE


Rais Kikwete akiweka jiwe la msingi kuashiria kuzindua rasmi ujenzi wa Daraja la Kigamboni katika hafla iliyofanyika huko Kurasini jijini Dar es Salaam leo mchana. Kushoto ni Waziri wa Ujenzi Dkt. Magufuli na wa pili kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Dkt. Ramadhani Dau. NSSF itagharamia asilimia 60 za ujenzi wa daraja hilo na Serikali asilimia 40. (Picha: Freddy Maro/IKULU)

 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete jana, Alhamisi, Septemba 20, 2012, ameweka Jiwe la Msingi la ujenzi wa Daraja la Kigamboni, Dar es Salaam kwa kuwaonya watu ambao amewaeleza kuwa wanavyo viwanda vya kutunga uongo kuacha tabia hiyo na kuelekeza nguvu kwenye maendeleo.

Aidha, Rais Kikwete amewahakikishia wakazi wote wa Kigamboni ambao wanaondolewa katika maeneo yao kwa ajili ya kupisha ujenzi wa daraja hilo na ujenzi wa Mji Mpya wa Kigamboni kuwa watalipwa stahili na haki zao zote.

Daraja hilo la Kigamboni ambalo wazo la kujengwa kwake lilibuniwa kwa mara ya kwanza zaidi ya miaka 30, tokea mwaka 1978, wakati wa uongozi wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, linajengwa kwa gharama ya Sh. bilioni 214.6 na litakuwa tayari katika muda wa miezi 36 ijayo, ingawa muda huo unaweza kupungua na kubakia miezi 30.

Daraja hilo ambalo litakuwa na urefu wa mita 680 linagharimiwa kwa pamoja na Serikali na Shirika la Hifadhi ya Jamii la NSSF ambalo litachangia kiasi cha asilimia 60 na Serikali asilimia 40.

Daraja hilo ambalo litakuwa na jumla ya barabara za kupitisha magari sita kwa wakati mmoja linajengwa na makampuni mawili ya China ambayo ni China Railway Construction Engineering Group na China Railway Major Bridge Engineering Company na mhandisi msimamizi wa ujenzi huo ni Kampuni ya Misri.

Daraja hilo litapunguza adha ya usafiri kati ya Kigamboni na Dar es Salaam ambao kwa sasa unategemea vivuko, ama boti ndogo, mitumbwi ama wenye magari kulazimika kufanya mzungumo wa kilomita 52. Kwa uamuzi wa sasa, wavuka kwa miguu ambao watakuwa na njia maalum kwenye daraja hilo pamoja na waendesha baiskeli watavuka bure bila malipo yoyote.

Akizungumza kwenye sherehe hiyo, Rais Kikwete amesema kuwa Serikali haiwezi kudhulumu wananchi wake na hivyo watu wote ambao wanastahili fidia kutokana na ujenzi wa daraja hilo na mji mpya wa Kigamboni watalipwa haki na stahiki zao.
Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa Serikali yake haitaruhusu mtu yoyote kuzuia ama kuchelewesha miradi ya maendeleo ambayo inalenga kunufaisha watu wengi.

Rais Kikwete pia amewaonya watu ambao wamelifanya suala la kutunga na kusema uongo kama sehemu ya utamaduni wao. “Watu wana viwanda vya kuzalisha uongo. Wanashinda wanasambaza uongo kwenye mitandao, kila mahali. Wamepata hata kusema kuwa mimi nimemuuzia George Bush eneo la Kigamboni. Bush aje kufanya nini Kigamboni?”

Rais pia amesema kuwa wapo watu ambao hawapendi maendeleo ya nchi. “Wanatamani kila siku tushindwe kuwaletea wananchi maendeleo. Lakini watakufa kwa kihoro kwa sababu hatutashindwa. Kila tulilosema tutalifanya, litafanyika”.

Amesema kuwa thamani kubwa ya vyama vya siasa ni maendeleo ya wananchi. “Lakini wapo wenzetu ambao wanaudhika wakiona maendeleo. Wanapenda hata daraja hili lisijengwe. Leo hawatalala usingizi. Kazi ya vyama vya siasa ni kuweka maslahi yetu sote mbele.”

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
20 Septemba, 2012

WAISLAMU KUKUSANYIKA JANGWANI KUPINGA FILAMU YA INNOCENCE OF MUSLIM

Amiri wa Shura ya maimamu Tanzania, Shekh Mussa Kundecha (kulia) akiwa masheikh wa Taasisi ya Umoja wa Wanazuoni wa Kiisilam  wakati wa kutangaza hatua ambazo waislamu watazichukua ili kupinga  Filamu iliyotengenezwa nchini Marekani ya kumkashifu Mtume Mohamad (SAW).Alitangaza
Msimamo uliotangazwa na waislamu hao katika mkutano huo  ni wakufanyika mkutano mkubwa  kwenye viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam ambapo waisilamu wote watakusanyika hapo kulaani Filamu hiyo.

Hawa ni waislamu waliohudhuria mkutano huo kwenye msikiti wa Kichangani jijini Dar es Salaam wakati wa Sala ya Ala -asiri leo, wakifuatilia kwa makini matamko na mawaidha ya masheikh mbalimbali

Friday 14 September 2012

SERIKALI IIGE MFANO HUU


Shamba la kilimo cha umwagiliaji cha Mbogamboga la Ngongoseke lililoko katika kijiji cha Nsola wilayani Magu ni mfano wa kuigwa katika matumizi ya ziwa Victoria. Pichani, nyanya ndogondogo maarufu kwa jina la nyanyapori zikiwa zimelimwa kitalaam kwenye shamba hilo ambalo, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alilitembelea Septemba 13, 2012. (Picha: Ofisi ya Waziri Mkuu)


SERIKALI YATONYWA

Programme Manager kutoka Zambia Bw, Bou Muchaba Iwa akisikiliza kwa makini katika mkutano huo

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Muungano wa Mashirika yasiyo ya kiserikali (TANGO) akizungumza na wadau mbalimbali lambapo ameishauri serikali kuongeza  uwekezaji    katika huduma za jamii  nchini kuliko kuwekeza zaidi kwenye uchumi.Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Muungano wa mashirika yasiyo ya serikali (TANGO),Bw.Ngunga Tepani katika mkutano wa wadau wa kupinga umasikini (SADC Regional Poverty Observatory) yaliyofanyika katika Hoteli Ya Blue Pearl.


Thursday 13 September 2012

KIONGOZI WA FREEMASON KUMWAGIKA LEO CLOUDS TV

Anndy Chande; Gerald Hando aliyeshika kikombe cha chai (kikombe mkononi)
Kinara wa kundi la Freemasons katika eneo la Afrika Mashariki, Jayantilal Keshavji Chande maarufu kama Sir Andy Chande, leo  kuanzia saa 3:00 usiku ataanika mambo mengi kuhusiana na undani wa kundi hilo wakati atakapozungumza na mtangazaji Gerrard Hando wa kituo cha televisheni cha Clouds "The Peoples Station".

Akizungumza kupitia kipindi cha Power Breakfast cha redio ya Clouds FM leo asubuhi, mtangazaji Hando ambaye ndiye aliyefanya mahojiano na Sir Chande, amesema kuwa mambo mengi kuhusu undani wa Freemasons na namna wanavyofanya kazi zao, yameelezewa kwa kina na kigogo huyo wa zamani wa kundi hilo duniani.

Amesema kuwa mahojiano hayo yatarushwa kuanzia leo kupitia kipindi chao kipya kiitwacho "The Interview', ambacho kitarushwa kuanzia leo usiku.

Namna ya kujiunga na Freemasons na mahala liliko hekalu la kundi hilo jijini Dar es Salaam ni miongoni mwa mambo yanayotarajiwa kuzungumziwa na Sir Chande.

Kigogo huyo wa Freemasons amekuwa karibu sana na viongozi wa juu serikalini, wakiwamo marais wastaafu wote wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Benjamin William Mkapa na sasa, Rais Jakaya Kikwete.


WALIMU WAPINGA KAMATI ILIYOTEULIWA NA SERIKALI


Chama cha walimu Tanzani CWT kimeitaka serikali kuacha kuwadanganya kama watoto  kufuatia Serikali kuzindua Baraza la pili la majadiliano ya pamoja kwenye utumishi wa  walimu lililozinduliwa jana  na Naibu waziri wa Elimu na Mafunzo  ya Ufundi  Mhe, Nlugo  na kuhudhuriwa na  wawakilishi wa CWT. Ambapo CWT imesema kuwa Baraza hilo halina mamlaka ya kutatua migogoro  sehemu ya kazi au migogoro  iliyokwisha jitokeza baina ya Watumishi wa Serikali na Serikali.


Rais wa CWT Bw, Gratian Mukoba  amesema  leo wakati anaongea na waandishi wa Habari kuwa  Kazi ya Baraza hilo ni kuishauri serikali kuhusu njia mbalimbali za kuzuia kutokea kwa migogoro na hiyo ni kwa mujibu  wa kifungu cha Sita cha Sheria ya majadiliano  ya pamoja  kwenye utumishi wa umma ya mwaka 2003 pamoja na kanuni zake za mwaka 2005.


Amesema kuwa  Chombo pekee chenye uwezo wa kushughulikia migogoro ni Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) ambapo chama kilipeleka mgogoro wake na kufikia hatua ya kutoelewa.
Ameishauri Serikali  kufungua upya jalada la majadiliano kwani chama kinaamini kuwa walimu wamerudi kazini wakiwa hawana ari ya kufanya kazi  kwani wanasubiri majadiliano kufanyika  kwa ajili ya mwaka ujao wa Fedha, hivyo ili kuwatia Moyo walimu  na kuwaongezea ari ya kufanya kazi  madai yao yanahitaji kusikilizwa ndani ya mwaka huu wa Fedha.