Friday 5 October 2012

WEZI WA UMEME WABABWA


 
WATU watano wamekamatwa kwa makosa ya wizi wa umeme, wakitumia  njia za kuharibu mita na kujiunganishia huduma hiyo bila ya kufuata taratibu za Shirika la Umeme nchini (Tanesco). 
Msimamizi wa operesheni ya ukaguzi wa mita uliyofanyika Temeke, Dar es Salaam  juzi,  Johari Nasibu, aliwaeleza waandishi wa habari kuwa jumla ya nyumba 80 zilifanyiwa ukaguzi na baadhi ya hizo kukutwa na makosa hayo.
Alisema  miongoni mwa makosa waliyotwa nayo wateja hao watano ni pamoja na wizi kujiunginishia umeme nje ya mita na kuchezea mita kwa kuziharibu ili ziweze kuandika matumitumizi stahiki.
“Kama tunavyofanya siku zote kwenye kazi  hii leo hii tumefanya hapa Mtoni eneo la Relini, tumefanikiwa kukuta mita nane zikiwa na makosa mbalimbali na hatua za haraka tulizo zichukua ni kuwasitishia huduma  kwanza kabla ya kufanya tathmini ya hasara tuliyopata ili waweze kutulipa na kama hawajalipa tunawafikisha mahakamani” alisema Nasibu.
 Johari alisema kiasi kikubwa cha umeme kimekuwa kikiibiwa na baadhi ya watu ambao siyo waaminifu huku  shirika hilo likiingia hasara bila kutarajia.
Aidha, shirika hilo linatarajia kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wale wote iwapo watabainika mojamoja kwa moja na kujihusisha vitendo vya kulihujumu shirika hilo.
Akifafanua kuhusu  utaalamu unaotumika ili kukotoa na  kugundua kiwango cha umeme kinachoibwa  na wateja wasiokuwa waminifu  Mmoja wa wakaguzi kwenye operesheni hiyo, Omari Mgasa, alisema kazi hiyo nirahisi kutokana na kuorodhesha idadi ya vifaa vyote vinavyotumia nishati hiyo katika nyumba pamoja na kuangalia kiwango cha matumizi ya mteja katika kipindi chote tangu alipounganishiwa huduma hiyo.
Pamoja na mafanikio ya operesheni  hiyo ya ukaguzi wa mita, alisema bado opersheni hiyo inakabiliwa na  changamoto mbalimbali, moja wapo ikiwa nikukosekana ushirikiano wakutosha  kwa  baadhi ya wateja ambao kwa makusudi wamekuwa wakifunga nyumba zao na kukimbia pindi wawaonapo wafanyakazi wa shirika hilo hasa wanapoandamana na askari polisi.
Katika hatua nyingine, Mgasa alisema kuna baadhi ya  maeneo ambayo wateja wanaotuhumiwa kufanya vitendo vya hujuma kwa kuiba umeme, shirika limepokea taarifa hizo ambapo limefika katika maeneo hayo na kusitisha huduma kwa wateja hao ikiwa ni pamoja kuwakatia nya kwenye nguzo kwa ajili ya hatua nyingine.

No comments: